Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Dk Harrison Mwakyembe amewashukuru viongozi wote wa Serikali, sekta binafsi, taasisi za Kidini vyombo vya habari na watanzania wote waliomfariji katika msiba wa mke wake.
Linah Mwakyembe amefariki dunia 15 mwaka huu katika hospitali ya Kairuki kwa ugonjwa wa saratani ya titi.
Mwakyembe amesema kuwa amefarijika sana kwa upendo ulioonyeshwa na kila mtu kwa nafasi yake katika kipindi hiki kigumu na kuahidi kuendelea kushirikiana nao katika kila jambo.
“Mimi na wanangu tumefarijika sana kwa kuona jinsi ambavyo watanzania na wana Kyela mlivvyokuwa na upendo kwetu mmetupa faraja na mmetutia nguvu na mmetuonyesha ushirikiano mkubwa katika jambo hili tunaomba mwenyezi Mungu awabariki sana na asanteni sana”Amesema Waziri Mwakyembe.
Kwa Upande wake Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Amos Makala amesema wananchi wa Mbeya watamkumbuka marehemu kwa moyo wake wa kujitolea kusaidia jamii katika mambo mbalimbali ikiwemo kufundisha jamii kumcha Mungu pamoja na Ujasiriamali uliosaidia wanawake wa Kyela kujiajiri.
No comments
Post a Comment