Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Friday, July 21, 2017

Madonna azuia kupigwa mnada barua ya mahusiano yake na Tupac Shakur.

Jaji mmoja nchini Marekani amesitisha mnada wa vitu binafsi vya mwanamuziki Madonna baada ya kusema kuwa haki yake ya faragha ilikiukwa.

Jaji wa mji wa New York Gerlad Lebovits aliamuru kesi hiyo kusikizwa kikamilifu mnamo mwezi Septemba tarehe 6, akilizuia jumba litakalofanya mnada huo la Gotta have Rock kuendelea na biashara hiyo.

Chupi ya Madonna, kitabu cha hundi , kichana , picha na barua ya uhusiano kati ya msanii huyo na aliyekuwa mwanamuziki Tupac Shakur ni miongoni mwa vitu vilivyosimamishwa kupigwa mnada.
Madonna anasema kuwa vitu hivyo viliibwa na rafikiye wa zamani.

Barua hiyo ya Tupac ambapo Tupac anasema kuwa uhusiano wake na Madonna ulivunjika kutokana na ubaguzi wa rangi ilitarajiwa kuuzwa kwa dola 400,000.

Barua hiyo ni ya tarehe 15 mwezi Januari 1995 na iliandikwa na Tupac Shakur wakati alipokuwa akihudumia kifungo cha miezi 18 kabla ya kupigwa risasi na kuuawa.
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment