Writen by
sadataley
10:47 AM
-
0
Comments
Moto wa nyika nchini Ufaransa umelazimu karibu watu 10,000 kuhamishwa usiku ya kuamkia leo kwa mujbu wa maafisa.
Wazima moto wametumwa kupambana na moto huo karibu na maeneo la Bormes-les-Mimoses.
Mapema Ufaransa iliiomba majirani wake wa EU msaada zaidi kupambana na moto huo.
Karibu ekari 4,000 za ardhi zimeteketea katika pwani ya Mediterranean.
Katika eneo la Corsica mamia ya nyumba zimehamwa.
Kwa ujumla wazima moto 400 na wanajeshi wanaotumia maji wanajaribu kuuzima moto huo tangu Jumatatu.
Takriban wazima moto 12 wamejeruhiwa na polisi 15 kuathiriwa na moshi kutoka kwa moto huo.
No comments
Post a Comment