Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Wednesday, July 19, 2017

Marekani yazidi kuiwekea Iran vikwazo vipya

Marekani imetangaza vikwazo vipya vya kiuchumi dhidi ya Iran, kuhusiana na mpango wake wa silaha zake za kinuklia.

Marekani inasema kuwa, inawalenga pia baadhi ya watu mashuhuri au rasilimali, ambazo zinaunga mkono mpango huo wa silaha za kinuklia mbali na kikosi cha ulinzi chenye nguvu nyingi nchini Iran cha Republican Guards.

Hatua hiyo inatangazwa siku moja tu baada ya Ikulu ya White House kusema kuwa Iran imeanza kutekeleza mpango wa silaha za nuklia.

Taarifa hiyo pia ilikosoa hatua ya Iran ya kuunga mkono serikali ya Syria na makundi kama Hezbollah na Hamas.

Marekani ina wasi wasi kufuatia shughuli za Iran eneo la mashariki ya kati, zinazovuruga utulivu wa eneo hilo.

Pia iliilaumu Iran kwa kuendeleka mzozo ulio nchini Yemen kwa kuunga mkono waasi wa Houthi. Iran bado haijatamka lolote kufuatia hatua hizo za hivi punde.
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment