Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Wednesday, July 19, 2017

Madalali bandia 12 wakamatwa na Polisi Dar

Jeshi la Polisi Mkoa wa Kipolisi wa Temeke jijini dsm linawashikilia madalali bandia 12 wanaodaiwa kuendesha vitendo vya wizi wa shehena za bidhaa za mamilion ya fedha huku wakitumia malori yaliyowekwa namba bandia pamoja na nyaraka bandia ili kufanikisha wizi huo.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Temeke Giles Mroto akizungumza na wanahabari amesema watuhumiwa hao wamekamatwa baada ya kupata taarifa ya malori ya bidhaa za vifaa vya ujenzi na ngano vyenye thamani ya shilini milion 400 , ambayo yalichepushwa na watuhumiwa badala ya kupelekwa geita yalipelekwa mbeya na kufichwa.

Amesema watuhumiwa hao pia walibainika kuwa na mihuri,nyaraka bandia mbalimbali za ukaguzi wa mizigo lakini pia redio call ambapo baadhi yao walijifanya maafisa wa polisi katika kufanikisha wizi huo.

Aidha kutokana na kukithiri kwa wizi huo Kamanda mroto ametoa wito kwa wale wanaosafirisha mizigo ndani na nje ya nchi kwa kuwatumia madali au mawakala kuwa waangalifu.
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment