Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Thursday, April 27, 2017

Uwanja wa ndege Damascus wakumbwa na mlipuko

Mlipuko wakumba uwanja wa ndege wa Damascus

Mlipuko mkubwa umekumba eneo moja karibu na uwanja wa ndege wa Damascus kulingana na shirika la waangalizi wa haki za kibinaadamu nchini humo the Syrian Observatory for Human Rights.

Mlipuko huo uliokuwa mkubwa uliweza kusikika mjini Damscus, alisema Rami Abdel Rahman mkuu wa shirika hilo nchini Uingereza.

Uwanja huo wa ndege upo yapata kilomita 25 kusini mashariki mwa mji mkuu wa Syria.

Mlipuko huo ulifuatiwa kwa karibu na moto mkubwa.Hakuna habari zozote kuhusu majeraha.

Syria imekabiliwa na mapigano ya wenyewe kwa wenyewe tangu 2011.

Mzozo huo umewaua zaidi ya watu 320,000 na baada ya miaka sita hakuna suluhu ya kisiasa iliopatikana.
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment