Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Saturday, April 22, 2017

Rais Magufuli ateua Kamishna wa Madini na bosi wa PURA

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli, amemteua Mhandisi Benjamin Joel Mchwampaka kuwa Kamishna wa Madini.

Taarifa iliyotolewa leo na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi imeeleza kuwa uteuzi wa Mhandisi Benjamin Joel Mchwampaka umeanza tarehe 19 Aprili, 2017.

Kabla ya uteuzi huo, Mhandisi Benjamin Joel Mchwampaka alikuwa Kamishna Msaidizi sehemu ya uchimbaji mdogo wa madini.

Wakati huo huo, Mhe. Rais Magufuli amemteua Dkt. Adelardus Kilangi kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Mamlaka ya Udhibiti wa Mkondo wa Juu wa Petroli (Petroleum Upstream Regulatory Authority - PURA).

Dkt. Adelardus Kilangi ni Mkurugenzi wa Chuo Kikuu cha Mtakatifu Agustino Tanzania (SAUT) kampasi ya Arusha.

Uteuzi wa Dkt. Adelardus Kilangi umeanza tarehe 19 Aprili, 2017
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment