Writen by
sadataley
12:03 PM
-
0
Comments

Pichani Mpendwa wetu Jennifer Livigha
aliyekuwa Mmiliki wa Libeneke la Chinga One na Mwanachama wa TBN Enzi za
uhai wake. Marehemu alizaliwa 25.01.1979 Nachingwea, alifariki nyumbani
kwake kinyerezi 18.02.2017 Jijini Dar es salaam. Marehemu alikuwa
anasumbuliwa na ugonjwa wa Ini. Atapumzishwa katika nyumba yake ya
milele nyumbani kwao Nachingwea.
Baadhi ya waombolezaji wakiwa katika
Ibada ya kuaga Mwili wa Marehemu Jennifer Livigha aliyekuwa mmiriki wa
Blog ya Chinga One katika Hospitali ya Amana.
Waongozaji wa Ibada ya kuaga mwili wa Marehemu Jennifer
Waombolezaji wakiwemo baadhi ya wana Tanzania Bloggers Network (TBN) ambapo Marehemu Jennifer alikuwa mwanachama
Mmoja ya waombolezaji akitoa historia fupi ya Marehemu
Mmoja wa wanafamilia akitoa utaratibu kabla ya kuanza kutoa heshima za Mwisho kwa mpendwa wetu Jennifer
Baadhi ya wanachama wa Tanzania Bloggers
Network (TBN) wakiwa wanaaga mwili wa aliyekuwa mwanachama mwenzao
Marehemu Jennifer ‘Chinga One’
Baadhi ya ndugu wa karibu, Jamaa na Marafiki wakiwa wanaaga Mwili wa Marehemu Jennifer
Baadhi ya waombolezaji wakiwa wanaimba nyimbo za maombolezo
Baadhi ya wanafunzi wakilia kwa uchungu
Mwenyekiti wa TBN Joachim Mushi
(Aliyevaa T-Shirt ya Mistari) akiongea jambo kabla ya safari ya kuelekea
Nachingwea kwa mazishi.
Baadhi ya wana TBN wakiwa katika Msiba wa mwanachama mwenzao Marehemu Jennifer
Safari ya kuelekea Nachingwea ikiwa imeanza ..
Picha zote na Fredy Njeje wa TBN
No comments
Post a Comment