Mbunge wa viti
maalum Mkoa wa Iringa Ritta Kabati ( CCM) ameanza kusaidia Ujenzi wa
ofisi za Matawi za CCM katika kata mbali mbali za Jimbo la Iringa kama
sehemu ya kukijenga chama hicho.
Akizungumza Leo wakati wa kukabidhi mifuko ya saruji kwa Ujenzi wa ofisi
za Tawi Kigamboni na Ruaha ,Kabati alisema kuwa anafanya hivyo kama
njia ya kutekeleza ilani na maadhimio ya CCM .
Hata hivyo alisema kuwa ataendelea kusaidia Ujenzi wa ofisi hizo ili
kuona ndani ya kipindi kifupi cha miezi mitatu ama sita kila tawi kuwa
na ofisi yake ya tawi.
Alitaka wanachama wa CCM kushikamana na kuendelea na Ujenzi wa ofisi hizo pia shughuli nyingine za kijamii
Alisema amepata kuchangia mifuko ya saruji Tawi la Ruaha na Kigamboni
wakati ofisi ya Tawi la Kitwiru Mdau wa Ccm amejitolea kujenga ofisi
hiyo na kila tawi amechangia mifuko 10 ya Saruji. |
No comments
Post a Comment