Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Thursday, November 6, 2014

UN:Hatuna raslimali za kudhibiti Ebola

   
Tony Banbury
Mkuu wa Umoja wa Mataifa anayesimamia kitengo cha kukabiliana na Ebola magharibi mwa Afrika ameiambia BBC kwamba hana raslimali za kuuthibiti ugonjwa huo.
Tony Banbury amesema kuwa msaada zaidi unahitajika kwa haraka ,licha ya mchango wa Uingereza,Uchina,Cuba na Marekani.
Lakini alikuwa na imani ya kuafikia malengo ya asilimia 70 ya vitanda kwa visa vipya na asilimia 70 ya mazishi kufikia mwezi Disemba.
Idadi ya vifo vilivyothibitishwa na shirika la afya duniani ni 4,818.
Idadi hiyo imeshuka tangu WHO kuripoti takwimu hizo awali ambapo shirika hilo linasema limebadilisha vile takwimu hizo zinavyochukuliwa.
Lakini imesema kwamba katika mataifa yalioathirika vibaya na mlipuko huo ikiwemo Liberia,Sierra Leone na Guinea,maambukizi yameendelea hususan katika miji mikuu
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment