Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Sunday, November 9, 2014

Mfuko wa Ebola waahidiwa Afrika

    Ebola
Wafanyabiashara na makampuni mashuhuri ya Afrika wameanzisha mfuko wa dharura kusaidia nchi zilizoathirika na Ebola.
Mkutano wa mwanzo wa kuahidi msaada uliofanywa Addis Ababa, Ethiopia, umekusanya dola milioni 28.5.
Fedha hizo zitatumiwa kutuma wafanya kazi wa utibabu 1,000 kwenda Guinea, Sierra Leone na Liberia.
Benki ya maendeleo ya Afrika itasimamia mfuko huo.
Hatua hiyo ni sehemu ya msaada wa Umoja wa Afrika kwa nchi zilizoatthirika.
Akizungumza baada ya mkutano huo, mwenyekiti wa AU, Dlamini Zuma, alisema fedha zitazopatikana ni sehemu ya mradi wa muda mrefu wa kupambana na majanga kama hayo siku za mbele.
Na makampuni yanayotoa huduma kwa simu za mkononi za Afrika yamesema kuwa mwezi ujao yataanzisha kampeni ya kuwapa nafasi wateja wao kusaidia nchi zenye Ebola, kwa kutoa mchango kwa kutumia ujumbe wa simu, SMS.
Inaarifiwa kuwa Afrika ina wateja milioni 700 wa simu za mkononi.
Ijumaa, shirika la madaktari la kimataifa, MSF, lilisema idadi ya wagonjwa wepya nchini Liberia inapungua.
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment