Writen by
sadataley
12:37 PM
-
0
Comments
Marekani kuunga mkono demokrasia Myanmar
Kiongozi wa upinzani wa Myanmar's , Aug San Suu Kyi, ameelezea imani yake kwamba Marekani itaendelea kuinga mkono juhudi za kuimarisha democrasia katika nchi hiyo iliyokuwa ikiendeshwa kwa utawala wa kijeshi kwa zaidi ya nusu karne.
Akiongea kwenye mkutano wa pamoja na rais Barack Obama huko kwao Yangon, Aug San Suu Kyi amesema japo mabadiliko yanafanyika katika hali ngumu ameiomba Marekani isilegeze msimamo wake.Akikubaliana na kauli hiyo rais Obama amesema ni sharti juhudi zaidi ziongezwe ili kupata ufanisi zaidi wa kidemocrasia.
Marekani tayari iliuondoshea vikwazo vya kiuchumi utawala wa nchi hiyo licha ya hatua halifu za mabadiliko.
Aung San Suu Kyi amesema ni jambo lisilokubalika kuwa angali anazuiliwa kuwania uongozi wa nchi hiyo kwa sababu watoto wake walizaliwa ng'ambo.
Habari kwa hisani ya BBC swahili
No comments
Post a Comment