Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Saturday, October 25, 2014

Misri yatangaza hali ya hatari

   
Wanajeshi
Misri imetangaza hali ya hatari katika eneo la Sinai kufuatia kuuawa kwa takriban wanajeshi 31 baada ya mashambulizi mawili yaliyofanyika kwenye vizuizi viwili.
Hayo ndiyo mauaji ya wanajeshi wengi zaidi kuwai kutokea nchini Misri kwa miongo kadha ambapo siku tatu za maombolezi zimetangazwa.
Rais wa Misri Abdul Fattah al Sisi aliitisha mkutano wa baraza la usalama wa kitaifa kujadili hali hiyo.
Wanajeshi 28 waliuawa kwenye shambulizi la bomu karibu na mji ulio kaskazini wa Arish huku wengine wakiuawa na watu waliokuwa na silaha kwenye kizuizi kimoja kilicho eneo hilo.
Mashambuli kutoka kwa makundi ya Jihad yanayolenga vituo vya usalama eneo la Sinai yameongezeka tangu jeshi limuondoe madarakani rais Mohamed Mosri mwaka uliopita.
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment