Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Sunday, October 26, 2014

Mali haitafunga mpaka wake na Guinea

    Mwanamke wa Mali anakaguliwa kama ana Ebola
Rais wa Mali anasema atafanya awezalo kuepusha taharuki baada ya mtu wa kwanza kuthibitishwa na ugonjwa wa Ebola nchini humo.
Msichana wa miaka miwili aliyeingizwa Mali kutoka Guinea, alikufa kutokana na ugonjwa huo Ijumaa.
Rais Ibrahim Boubacar Keita alisema kisa hicho hakitamfanya afunge mpaka wa Mali na Guinea.
Juhudi zinafanywa kuwatafuta na kuwaweka karantini watu wote waliomkaribia msichana huyo.
Na Shirika la Afya Duniani, WHO, linasema kuwa idadi ya watu waliothibitishwa rasmi kupata Ebola imepindukia 10,000 ingawa inafikiriwa kuwa idadi halisi ni zaidi sana ya hiyo.
Watu kama 5,000 wamekufa kutokana na ugonjwa huo hadi sasa.
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment