Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Friday, July 25, 2014

Tanzania yang’ara kuogelea


Muogeleaji wa Tanzania, Mariam Ali Foum akimaliza raundi ya kwanza ya mchezo wa kuogelea kwa wanawake wa urefu wa mita 50 kwa mtindo wa Breaststroke. iFoum ni mmoja wa waogeleaji wa Tanzania wanaoshiriki Michezp ya Jumaiya ya Madola mjini Glasgow. Picha na AFP      
Na Imani Makongoro, MwananchiDar es Salaam. Muogeleaji  wa Tanzania, Ammaar Ghadiyali amefanikiwa kuingia hatua 16 bora ya  Michezo ya Jumuiya ya Madola baada ya kuongoza kwenye mbizi za mita 50 hapo jana.
Ghadiyali amekuwa Mtanzania wa kwanza kwenye michezo hiyo kuongoza katika mchujo wa mchezo wa aina ya  butterfly akitumia sekunde 28:11 kwenye bwawa la kuogelea la kituo cha Tollcross nchini Scotland na kumaliza katika nafasi ya kwanza.
Meneja wa Tanzania kwenye michezo hiyo, Muharami Mchume aliiambia Mwananchi jana kwa simu akiwa Glasgow kuwa, matokeo ya waogeleaji hao yameongeza morali kwa wachezaji wengine na wanaamini kuwa wanaweza kufanya vizuri na kurejea na medali.
“Wote wanasema wana deni kama Rais Kikwete (Jakaya) alivyowaambia kila mmoja ana ari ya ushindani.
Japo wenzetu wawili wa judo tayari wameondolewa, hiyo haijawaathiri wengine katika kambi yetu hasa baada ya waogeleaji kuanza vizuri,” alisema Mchume.
Mbali na Ghadiyali, muogeleaji mwingine wa Tanzanian, Hila Hemed alishika nafasi nne katika mchujo huo wa kuogelea kwa mtindo wa butterfly.
Kwa mujibu wa Mchume, Ghadiyali tayari ameingia hatua ya 16 bora na Mariam alimaliza wa pili akitumia muda wa sekunde  37.11 na sasa anasubiri matokeo ya mchujo ya makundi mengine ili kuweza kuingia hatua hiyo kwenye staili hiyo.
Tayari wana judo, Abubakari Nzige na Ahmed Magogo wameaga kwenye mashindano hayo.
Nzige alipoteza pambano lake dhidi ya Mohamed Fakri wa Malaysia kwenye uzani wa kg 66 wakati Magogo akiwa ameshindwa kucheza pambano lake na kumpa ushindi Daniele Grance wa Afrika Kusini ambaye atacheza hatua ya 16 bora dhidi ya Mghana, Razak Abugiri.
Mchume alisema bado judo ina nafasi ya kufanya vizuri kwa wachezaji waliosalia wa Mbaruku Seleiman atakayecheza leo katika hatua ya 16 bora dhidi ya mshindi Dodge na Leat.
“Mbali na judo na kuogelea, tunaamini wachezaji wetu wa mpira wa meza na kunyanyua vitu vizito watafanya vizuri kwenye michezo yao.
“Pia, mabondia, Seleman Kidunda na Emmilian Patrick watacheza kesho (leo) na hivi sasa (jana mchana) wanashiriki zoezi la kupima uzito na afya,” alisema Mchume.
Wanariadha Fabiano Joseph na John John Leonard wataanza harakati za kusaka medali leo katika mbio ndefu,  huku Alphonce Simbu, Fabian Sulle na Wilbaldo Peter watachuana kwenye mita 5,000) kwenye uwanja wa Hamden Park.
Mara ya mwisho Tanzania kupata medali kwenye michezo hiyo ilikuwa 2006 nchini Australia ambako ilitwaa medali mbili. Mwaka 1970 ilitwaa medali ya kwanza kwenye michezo hiyo iliyochukuliwa na bondia Titus Simba (ambaye sasa ni marehemu).
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment