Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Wednesday, July 16, 2014

Semina kuzuia kupanga matokeo


Timu ya taifa ya Tanzania
Kituo cha Kimataifa cha Ulinzi wa michezo (International Centre for Sport Security) wiki hii kitatoa elimu kuhusu kupiga vita upangaji wa matokeo kwa wanamichezo vijana wa kiafrika.
Kama njia mojawapo ya Kituo hicho kubeba mzigo wa kuwaelimisha wachezaji vijana kuhusu madhara ya kupanga matokeo , Stuart Page Mkurugenzi Mkakati na maendeleo ya sera wa Kituo hicho na Jake Marsh, Mchunguzi wa kituo hicho , wataongoza warsha ya siku tatu itakayohusu namna ya kurejesha hadhi kupiga vita upangaji matokeo kwa wachezaji vijana na maafisa watakaoongozwa na viongozi wa chama cha soka Tanzania, kikiwemo Chama cha Soka Tanzania, mradi wa Kampuni ya Symbion/Sunderland AFC ambayo ni kampuni binafsi ya kwanza barani Afrika inayomiliki chuo cha soka pamoja na chuo cha michezo cha watoto wa mitaani kilichopo Tanzania.
Warsha hiyo ina lengo la kufundisha wanamichezo vijana wenye umri kati ya miaka 12 hadi 18 wanaotoka katika vyuo vya michezo pamoja na watoto wa Tanzania wanaoishi maeneo hatarishi.
Warsha hiyo itaanza kwa kuwafundisha wachezaji wa timu ya taifa ya Tanzania walio chini ya Umri wa miaka 17 katika uwanja Karume mjini Dar es Salaam nchini Tanzania.
Wachezaji watakaohudhuria semina hiyo watajifunza mada mbali mbali ikiwemo namna ya kuzuia kupanga matokeo na kuinua vipaji vya wachezaji vijana, mbinu za kubaini, kuzuia na kuripoti mpango hiyo na namna ya kuonya kuhusu mipango hiyo hatari ya kupanga matokeo.
Stuart Page wa Kituo hicho cha Kimataifa anasema " Elimu na Kinga ndio msingi wa Kituo hicho kuondoa matatizo ya upangaji wa matokeo na hasa wanariadha ndio msingi wa mkakati wa kituo hicho."
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment