Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Saturday, July 12, 2014

REKODI: Minziro: Sitasahau kipigo cha Simba


Fred Minziro       
Na Oliver Albert, MwananchiDar es Salaam. Kocha wa JKT Ruvu, Fred Felix Minziro amesema katika maisha yake ya ukocha hatasahau kipigo cha mabao 5-0 walichokipata  Yanga kutoka kwa Simba, msimu wa 2011/2012.
Akizungumza na gazeti hili katika mahojiano maalumu jana,  Minziro alisema: “Nilifungwa mabao 5-0 na Simba nikiwa nimebaki kocha peke yangu katika benchi maana kocha mkuu Kostadin Papic aligoma na kukaa jukwaani.
“Ilikuwa ni mechi iliyoshusha heshima ya klabu, iliyotia simanzi na ambayo iliweka rekodi mbaya katika maisha yangu ya ukocha,  ndiyo maana mpaka sasa imebaki mawazoni mwangu, sitakuja kuisahau,” alisisitiza.
Aliongeza: “Iliniuma sana siku ile kwani matokeo yalipangwa, yaani mechi ile imebaki kwenye kumbukumbu yangu kwani hata magoli yenyewe yaliyofungwa, yaani magoli yote yalipangwa siyo siri na hakuna asiyefahamu hilo.
“Kipindi kile Yanga ilikuwa na mgogoro wa uongozi, hivyo mechi ilipangwa tufungwe ili viongozi waonekane hawafai hasa mwenyekiti wa wakati huo,    Lloyd Nchunga na lengo lao wamwondoe, lakini mimi nasema walimwonea kwani alikuwa ni kiongozi mzuri, ila ile mechi sitakaa niisahau.”
Aliongeza :”Ukiangalia ile mechi jinsi wachezaji walivyokuwa wanacheza unaona kabisa matokeo yalipangwa, wachezaji wangu walicheza chini ya kiwango kuliko siku zote, unaona mabeki hawakabi, viungo hawapambani, washambuliaji ndio kabisa hawakuonyesha  kuwa  wanataka kufunga, yaani ilionyesha dhahiri kuna kitu kilipangwa. Sijui kulikuwa na maelekezo, lakini sijui  walipata wapi maelekezo hayo.”
Minziro alikuwa beki mahiri wa Yanga pia kocha msaidizi wa klabu hiyo kabla ya Desemba mwaka jana kufukuzwa akiwa  pamoja na kocha mkuu, Mholanzi, Ernest Brandts.
Hata hivyo, Minziro aliwausia wachezaji waache kutumika kama chambo kutoka kwa baadhi ya watu na kucheza chini ya kiwango kwa maelekezo ya viongozi fulani kwani jambo hilo linashusha heshima zao.
 “Ninachowashauri wachezaji  wacheze mpira hata kama kuna mgogoro  katika uongozi hawapaswi kuingilia hilo hata wakiambiwa  wacheze chini ya kiwango wao wanatakiwa kucheza kama siku zote ili kutoharibu CV zao kwani ile mechi kuna wachezaji walijiharibia kabisa mpaka  sasa wamepotea katika ramani ya soka,” alisema.
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment