Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Saturday, July 19, 2014

Dk Slaa: Tulishinda urais 2010


Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe (Kulia) akiteta jambo na Katibu Mkuu wa chama hicho, Dk Willbrod Slaa wakati wa kikao cha Kamati Kuu kilichofanyika jana Dar es Salaam. Picha na Venance Nestory      
Na Mwandishi Wetu, MwananchiDar es Salaam. Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kimesema kuwa kinaamini kilishinda uchaguzi wa rais katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2010 chini ya mfumo wa vyama vingi.
Katibu Mkuu wa Chadema Dk Willbrod Slaa, ambaye pia alikuwa mgombea urais kwa tiketi ya chama hicho kwenye uchaguzi huo, alibainisha hayo hivi karibuni wakati wa mahojiano maalumu na waandishi wa gazeti hili.
Dk Slaa alisema kuwa ana uhakika kuwa chama chake kilipata kura nyingi zaidi za urais, tofauti na mgombea wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Jakaya Mrisho Kikwete aliyetangazwa mshindi.
“…Baada ya uchaguzi wa mwaka 2010, tulikataa kumtambua Rais Kikwete, ingawa wakati ule hatukujua kwa uhakika kama tulishinda. Kadiri nilivyozunguka, ndiyo kadiri tulivyoanza kuamini kwamba tulishinda,” alisema Dk Slaa.
Alisema kuwa takwimu walizonazo zinaiaminisha Chadema kwamba ilishinda Uchaguzi Mkuu wa urais mwaka 2010.
“Sababu, unafika kwenye jimbo wanakusomea kura ulizopata katika uchaguzi ule wakizilinganisha na alizozipata Kikwete na Profesa Ibrahim Lipumba… wanasema Dokta hapa ulimshinda… kwa kura 20,000, pale ulimshinda kwa kura 15,000 pale ulimshinda kwa kura…,” alifafanua na kusisitiza:
“Sasa ndiyo, tuna uhakika kama tulishinda na ndiyo maana Kikwete hajawahi kwenda kwa wananchi kushukuru kwa kumchagua, tofauti na tabia yake. Anachofanya sasa ni kwenda kuzindua miradi.”
Hata hivyo, Dk Slaa alisema hawakuweza kuendelea na madai yoyote kwa sababu kwa mujibu wa Sheria na Katiba ya nchi, mshindi wa urais akishatangazwa hairuhusiwi kupinga kwa namna yoyote hata mahakamani, akieleza kuwa hiyo pia ndiyo sababu ya kuhitaji Katiba Mpya.
Tume ya uchaguzi na CCM
Alipoulizwa kuhusu tuhuma hizo, Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (Nec), Jaji Mstaafu Damian Lubuva alisema anasubiri kwanza kusoma kwenye vyombo vya habari alichokisena Dk Slaa ndiyo ataweza kuzungumzia suala hilo.
“Kwa kuwa wewe ndiyo umeniambia Dk Slaa amesema hivyo, ngoja nione kwanza halafu tume itatoa maelezo,” alisema Jaji Lubuva.
Alipopigiwa simu Makamu Mwenyekiti wa CCM- Bara, Philip Mangula ili atoe ufafanuzi kuhusu suala hilo, alimsikiliza mwandishi wetu, kisha akasema yupo katika kikao na kukata simu.
Kwa habari zaidi ingiahttp://www.mwananchi.co.tz/habari/Kitaifa/Tulishinda-urais-2010/-/1597296/2389694/-/8ximoi/-/index.html
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment