Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Friday, May 16, 2014

MUUJIZA: MAMA AKUMBATIA MAITI YA KICHANGA CHAKE HADI KIKAFUFUKA

Kate na Davie Oggs wakiwa na kichanga chao. ©Howlifebegan/youtube
Hakuna furaha kubwa kwa mjamzito kujifungua salama, mtoto aliye na afya njema. Na hakuna majonzi makuu kwa mjamzito kupoteza kichanga chake kwa sababu yoyote ile, ikiwemo kuibiwa ama kufuariki.
Kilichotokea kwa mama huyu huko Sydney, (Autsralia) anayefahamika kwa jina la Kate hakika hakielezeki kwa urahisi. Akiambatana na mume wake, Daid Ogg - walifika hospitalini hapo ambapo mama huyo alijifungua watoto mapacha kabla ya muda muafaka, ambapo walikaa tumboni kwa kipindi cha miezi 6 tu.
Pacha wa kike, Emily alinusurika, wakati pacha wa kiume, Jamie, alitangazwa na daktari kuwa amefariki punde tu baada ya kuzaliwa. Katika hali ya majonzi, mama wa kichanga hicho, Kate - alishika mwili wa kichanga chake hicho, huku akikiongelesha pamoja na mumewe licha ya kwamba walishafahamishwa kuwa hauna uhai (a lifeless body) - kwa kukitajia jina la dada yake, na kwamba anaendelea vizuri, huku pia wakimuita kwa jina lake (japo hasikii)

Kwa masaa mawili wazazi hao waliuongelesha mwili wa kichanga hicho ambacho hakikuwa na pumzi, na baada ya muda huo kila mtu akabaki ameduwa baada ya kichanga hicho kufungua macho na kuungana na familia hiyo ambayo ilijawa na furaha ya ajabu, ambapo wanaeleza tukio hilo kwamba si kingine bali ni muujiza.
Hakika hapo pia tunakumbushwa kuwa maneno yana nguvu ya kuumba ama kubomoa, jambo gani unalisema kwa mtoto wako ama mwenza wako? Mjenge kwa namna ambavyo anatakiwa kuwa, ikiwemo kumpa jina zuri na sio kumsema kwa namna alivyo.
HABARI KWA HISANI YA Gospel Kitaa
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment