Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Friday, May 16, 2014

BJP yaongoza katika Uchaguzi India

Chama cha BJP kinaongoza katika matokeo ya awali
Shughuli ya kuhesabu kura imeanza rasmi nchini India baada ya uchaguzi uliodumu kwa kipindi cha wiki tano.
Matokeo ya awali yanaashiria ushindi kwa muungano unaoongozwa na mgombea wa upinzani Narendra Modi aliayeahidi nafasi za ajira na maendeelo ya kiuchumi.
Kuna hali ya shangwe kwenye makao makuu ya chake cha BJP mjini Delhi kulikowekwa televisheni kubwa zinazoonyesha matokeo huku pia nyimbo zikiimbwa.
Hata hivyo utulizu umeshuhudiwa kwenye makao makuu ya chama tawala cha Congress.
Kiongoi kutoka kwa chama cha Congres Abhishek Manu Singhvi anasema kuwa matokeo yalioneka yasiyo na matumaini akiongeza kuwa hayo ndiyo matokeo mabaya zaidi kuwai kushuhudiwa na chama hicho.
Zaidi ya watu milioni mia tano walipiga kura na kuweka rekodi mpya wa wapiga kura ku asilimia sitini na sita.
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment