Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Tuesday, September 3, 2013

KWAYA YA SHANGILIENI YAZIDI KUJIDHATITI YANUNUA BASI LA PILI, KUZINDUA ALBUM MPYA JUMAPILI


Kwaya ya Tumaini kutoka kanisa Anglikana Mtakatifu James Kaloleni jijini Arusha imeendelea kujidhatiti katika suala zima la kuhubiri injili kwa njia ya uimbaji baada ya kufanikiwa kununua basi la pili la kusafiria aina ya Double Coaster huku wakitarajia kuweka wakfu kanda yao mpya ya sauti siku ya jumapili ijayo ya tarehe 8 kanisani kwao Kaloleni.


Kwaya hiyo ambayo inamiliki vyombo vya kisasa vya muziki, ilifanikiwa kununua basi miaka ya karibuni na sasa limefanikiwa kuongeza gari hilo la pili hali ambayo inaonyesha malengo waliyojiwekea kama kwaya yanaendelea kutimia. Kwa upande wa kanda mpya ambayo wanatarajia kuizindua jumapili hii wameipa jina la "Nisamehe" ikiwa na jumla ya nyimbo 10 zenye mahadhi tofauti, ambapo kuelekea tukio hilo, hapo jana waumini wa kanisa hilo waliweza kupata wasaa kwakusikiliza nyimbo hizo.

Mabasi ya kwaya ya Tumaini yakiwa yameegeshwa eneo la kanisa St.James.
Wanakwaya na waumini wa kanisa la St.James wakifuatilia ujio wa album mpya ya Tumaini wakati wa ibada jana.

Habari na Gospel Kitaa
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment