Writen by
sadataley
6:50 PM
-
0
Comments
Askari polisi saba wanahojiwa na wachunguzi nchini Kenya, wakishukiwa kuhusika na uporaji wakati wa moto ambao uliteketeza eneo la mapokezi la uwanja wa kimataifa mjini Nairobi mwanzo wa juma.
Askari hao, akiwemo inspector, wanashutumiwa kuiba pesa na ulevi.
Wafanyakazi wa uwanja wa ndege, uhamiaji na madereva wa taxi ni kati ya wale wanaohojiwa, baada ya kamera za usalama kuonesha watu wakiiba vitu madukani.
Wakuu piya wanawatafuta watu wane waliokuwa wakisubiri kufukuzwa nchini kabla ya moto huo kutokea.
Watu hao wametoweka.
Ijumaa Rais Uhuru Kenyatta alisema moto huo haukutokana na kitendo cha kigaidi.
Imewekwa na Happy Adam
No comments
Post a Comment