Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Tuesday, August 20, 2013

Kesi ya Oscar Pistorius ni mwaka ujao

Mwanariadha mlemavu wa Afrika Kusini Oscar Pistorius amefika mahakamani ambapo ameshtakiwa kwa mauaji ya mpenzi wake.
Oscar Pistorius
Mahakama imemsomea makosa ya kumuua,Reeva Steenkamp. Kesi dhidi ya mwanariadha huyo itaanza Mwezi Machi mwaka ujao.
Oscar Pistorius alizingirwa na umati mkubwa wa waandishi wa habari alipofika mahakamani mji wa Pretoria. Akiandamana na jamaa wake mwanariadha huyo alifanya maombi maalum. Punde baada ya kusomewa makosa ya kumuua Mwanamitindo Reeva Steenkamp, Oscar alionekana kupatwa na huzuni kubwa.
Kesi hiyo sasa imehamishiwa mahakama kuu na itasikizwa mapema mwakani.Pistorioua anadaiwa kumpiga risasi mpenzi wake usiku wa manane akiwa amejifungia choo ya nyumba yake.
Mwanariadha huyo amejitetea na kusema alidhania ni mtu mwingine aliyejaribu kuingia kwa nguvu ndani ya nyumba. Upande wa mashtaka umesema mwanariadha huyo alipanga kumuua mwanamitindo huyo.
Mmoja wa majirani wa Pistorius na ambaya ni shahidi alikiri kusikia mayoye ya mwanamke kisha milio ya risasi. Hata hivyo shahidi mkuu anayefahamu kilichotokea wakati huo ni mmoja tu naye ni Oscar Pistorius.
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment