Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Monday, April 2, 2018

Waziri mkuu wa Japan kukutana na Rais Trump mjini Florida

Waziri mkuu wa Japan Shinzo Abe amesema atakutana na Rais wa Marekani Donald Trump mjini Florida kati ya tarehe 17 hadi 20 mwezi huu kujadili masuala ya biashara, mpango wa kinyuklia na makombora wa Korea Kaskazini na suala la raia wa Japan wanaoshikiliwa mateka na Korea Kaskazini kwa miongo kadhaa sasa.

Abe anapanga kukutana na Trump kabla ya kiongozi huyo wa Marekani kufanya mkutano wa kihistoria na Kiongozi wa Korea Kaskazini Kim Jong Un mwishoni mwa mwezi Mei.

Abe amesema wanahitaji kuendelea na shinikizo dhidi ya Korea Kaskazini ili ichukue hatua madhubuti kuachana na mpango wake wa kinyuklia katika rasi ya Korea.

Mwezi uliopita, Trump aliongeza ushuru dhidi ya bidhaa za bati na chuma zinazoingizwa Marekani kutoka nje ambapo Japan ni miongoni mwa nchi zinazoathirika na ongezeko hilo la ushuru.
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment