Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Monday, February 24, 2014

Tutu amsihi Museveni kuhusu mswada mpya

Rais Yoweri Museveni
Askofu mstaafu wa Cape Town, Desmond Tutu, amemsihi Rais Museveni wa Uganda asitie saini mswada ulioleta utatanishi kuhusu wapenzi wa jinsia moja.
Akofu Tutu, aliyewahi kupata tuzo ya amani ya Nobel, alisema amevunjika moyo kuwa Rais Yoweri Museveni anaonesha kubadilisha msimamo wake, kwa vile awali alisema kuwa hataruhusu mswada huo kuwa sheria.
Desmond Tutu alisema haistahiki kuwa na ubaguzi kama huo, na alitoa mifano ya mfumo wa zamani wa ubaguzi wa rangi uliokuwako Afrika Kusini na ubaguzi wa Wa-Nazi wa Ujerumani.
Alisema hiyo ni mifano mibaya kabisa.
Awali mswada wa Uganda ulipendekeza kifo kwa vitendo vya kulawiti na baadae kubadilishwa kuwa adhabu ya kifungo.
Chanzo: bbc swahili
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment