Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Wednesday, December 18, 2013

Wabunge India wataka Marekani iwajibike

Wabunge wa India wameelezea kusikitishwa na kitendo cha kumkamata na kumtendea vibaya mmoja wa wanadiplomasia wake mjini New York wiki iliyopita.
Waandamanaji India wakipinga ubalozi wa Marekani
Kiongozi wa upinzani katika baraza la juu la bunge la India, Arun Jaitley amesema kukamatwa kwa balozi huyo ni ukiukaji wa mkataba wa Vienna.
Bi Devyani Khobragade, naibu balozi , alifungwa pingu na kupekuliwa akiwa amevuliwa nguo.
Bi Khobragade amekanusha tuhuma za udanganyifu wa viza na kutoa taarifa za uongo kuhusu tuhuma kwamba alikuwa anampunja mshahara mfanyakazi wake wa ndani.
Mfanyakazi huyo alilalamika kuwa balozi huyo alikuwa akimlipa kima cha chini cha mshahara kuliko kinachoelezwa katika viza ya Marekani.
Kufuatia kukamatwa kwake, Bi Khobragade alifikishwa mahakamani Ijumaa iliyopita na kuachiwa kwa dhamana.
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment