Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Saturday, April 7, 2018

TIMES FM NA CLOUDS FM ZAPEWA ADHABU KWA UKIUKAJI WA KANUNI ZA UTANGAZAJI.



Kamati ya Maudhui ya TCRA leo imetoa hukumu kwa vituo viwili vya radio Times FM radio na Clouds FM kwa makosa ya ukiukwaji wa Kanuni za   Utangazaji za mwaka 2018.

Times FM walitangazwa mahojiano na mwanamziki Nasib Abdul "Diamond Platinum" ambapo katika mahojiano hayo mwanamuziki huyo alitamka maneno yasiyofaa kimaudhui akimshambulia Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Juliana Shonza. 

Kufuatia hali hiyo, Times FM wamepewa Onyo na kutakiwa kumuomba radhi Mhe.Naibu Waziri Shonza na jamii kwa ukiukwaji huo wa maadili ya Utangazaji.


Kwa upande wa Clouds FM, kituo hicho kimepewa onyo kwa kutozingatia mizania ya utoaji wa habari uliohusu pande mbili ya mwanamuziki  Ibrahim Musa "Roma mkatoliki" na Naibu Waziri Mhe. Shonza.

kamerayangu.co.tz
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment