Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Monday, April 16, 2018

Okwi afikia magoli ya Tambwe, Bocco

Mshambuliaji Emmanuel Okwi wa Simba, leo amefunga bao lake la 19 katika Ligi Kuu Bara.

Okwi amefunga bao moja wakati Simba ikiitwanga Prisons kwa mabao 2-0 katika mechi ya Ligi Kuu Bara kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.

Bao la 19, linamfanya Okwi kufikia rekodi mbili za wafungaji Amissi Tambwe na John Bocco ambaye kwa sasa ni nahodha wake.

Bocco aliwahi kufunga mabao 19 na kufanikiwa kuwa mfungaji bora wa Ligi Kuu Bara na Tambwe akafanya hivyo na kuwa mfungaji bora.

Kwa kuwa Simba bado ina mechi nyingine sita, maana yake Okwi ana nafasi ya kufikisha mabao 20 au zaidi kama ataendelea kufunga tena.
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment