Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Saturday, July 22, 2017

Walichochukua polisi nyumbani kwa Lissu

Tundu Lissu

 Baada ya jeshi la polisi kumkamata Tundu Lissu siku ya Alhamsi uwanja wa ndege akiwa anaelekea nchini Rwanda. Jana jeshi hilo lilikwenda kufanya upekuzi nyumbani kwa Mbunge wa Singida Mashariki (CHADEMA) ambaye pia ni Mwanasheria Mkuu wa chama hicho.

Siku ya jana Ijumaa ya tarehe 21/07/2017  jeshi la polisi walimchukua Tundu Lissu na kwenda naye mpaka kwa Mkemia Mkuu wakiwa na lengo la kutaka kumpima mkojo kabla ya kuelekea nyumbani kwake kufanya ukaguzi. Lakini kiongozi huyo aligoma kufanya kipimo hicho kwa madai kuwa tuhuma anazotuhiwa haziendani na vipimo hivyo.

Kwa mujibu wa Tumaini Makene ambaye ni Afisa habari wa (CHADEMA) anasema kuwa jana polisi baada ya kufanya ukaguzi nyumbani kwa Tundu Lissu waliweza kuchukua CD 6 na kuondoka nazo.

"Jeshi la Polisi bado linamshikilia, Mhe. Tundu Lissu, Kwenye upekuzi jana nyumbani kwake walichukua CD 6 za 1996 zinazohusu masuala ya mgodi wa Bulyag'hulu, Shinyanga" ilisema taarifa ya CHADEMA

Leo ni siku ya pili toka kiongozi huyo anashikiliwa na jeshi la polisi Dar es Salaam lakini Wakili Peter Kibatala pamoja na Wakili Fatma Karume wa IMMA Advocates kwa upande wao wanasema wanaendelea na juhudi za kisheria kuhakikisha kiongozi huyo anapatiwa dhamana au kufikishwa mahakamani mapema iwezekanavyo.
Source: Eatv
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment