Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Thursday, July 27, 2017

Urusi yasema vikwazo vya Marekani vitaathiri uhusiano wao

Naibu waziri wa mashauri ya nchi za kigeni wa Urusi anasema kuwa, vikwazo vipya vya kiuchumi vilivyotolewa na Marekani, vitahujumu uhusiano bora ulipo kati ya Moscow na Washington.

Sergei Ryabkov amesema kuwa utayumbisha kabisa uhusiano wao.

Awali, baraza la wawakilishi la Marekani limepiga kura kwa kauli moja kuweka vikwazo vipya dhidi ya Urusi, Iran na Korea Kaskazini.

Urusi inaadhibiwa kutokana na kudaiwa kuingilia uchaguzi mkuu wa mwaka jana wa Marekani, huku Korea Kaskazini na Iran wakiadhibiwa kutokana na mipango yao ya kufanyia majaribio zana zao za makombora ya kinuklea.

Mswaada huo unatarajiwa kupitia kwa baraza la seneti, kabla ya kupelekwa kwa Rais Donald Trump ili audhinishe na kuwa sheria kamili.
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment