Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam Paul Makonda leo Julai 25 amefanya ukaguzi katika ujenzi wa jengo la wodi ya wazazi la ghorafa tatu kwenye Hospitali ya Amana Jijini Dar es salaam, ambapo ameridhishwa na ujenzi wa jengo hilo lililogharimu kiasi cha zaidi ya Sh. bilioni 1 na kuahidi kwamba katika siku zijazo atamuomba Rais Magufuli kuzindua jengo hilo.
Ufadhili wa ujenzi wa jengo hilo umetolewa na Kampuni ya Amsons ambao wamejenga kwa gharama zao.
Kukamilika kwa ujenzi huo kutasaidia wakina mama 150 watakaofikishwa katika hospitali hiyo kwa wakati mmoja.
|
Jengo wanalotumia Wazazi mpaka sasa Hospitalini hapo |
Kwa upande wake, Meneja wa ukuzaji biashara wa kampuni ya Amsons Group,Suleiman Amon, alisema ujenzi huo utakuwa na ghorofa tatu
Hata hivyo RC Makonda ametoa wito wa kutunzwa majengo hayo ili yaweze kudumu kwa muda mrefu, na magodoro yaliyoyolewa yatapunguza changamoto kwa wazazi ambao wamekuwa wakilala watatu hadi wanne katika godoro moja,” alisema.
No comments
Post a Comment