Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Friday, July 21, 2017

Msuva afanikiwa kwenda kuiongezea nguvu Taifa Stars

Baada ya kukwama jijini Dar es Salaam, hatimaye Msuva ameondoka kwenda Rwanda kuungana na kikosi cha Taifa Stars.

Stars iko jijini Kigali kuivaa Rwanda keshokutwa katika mechi ya kuwania kucheza michuano ya Chan. Katika mechi ya kwanza mjini Mwanza, timu hizo zilitoka sare ya bao 1-1.

Awali, Msuva alipanga kwenda Rwanda, jana alifika hadi Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JKIA), lakini baadaye alirejea nyumbani.

Lakini leo amefanikiwa kuondoka kwenda Rwanda kuongeza nguvu katika kikosi cha Stars.

“Kweli nimefanikiwa, nitaondoka leo jioni,” Msuva aliiambia SALEHJEMBE leo mchana.

« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment