Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Thursday, July 20, 2017

Kilichojiri baada ya Lowassa kufika kuhojiwa na DCI

 Waziri Mkuu wa zamani na Mjumbe wa Kamati Kuu ya CHADEMA Edward Lowassa leo July 20, 2017 ameripoti katika Ofisi ya Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai kuhojiwa ‘DCI’ kuhojiwa kwa mara ya nne.

Lowassa ametakiwa kurudi tena kwa DCI baada ya wiki tatu kutokana na kuwa upelelezi bado haujakamilika.

Lowassa ameambatana na mkewe, Regina na mwanasheria wake, Peter Kibatala.

Hii ni mara ya nne kwa Lowassa kuripoti hapo akituhumiwa kutoa kauli za kichochezi wakati wa futari iliyoandaliwa  Juni 23, na Mbunge wa Ukonga, Mwita Waitara.

Katika futari hiyo, Lowassa anadaiwa kutoa maneno ya uchochezi kuhusu masheikh wa Taasisi ya Uamsho wanaoshikiliwa gerezani  akidai utaratibu wa kisheria ufanyike ili waachiwe huru.

Polisi wameimarisha ulinzi eneo hilo, huku Lowassa akiwa ndani tayari kwa kuhojiwa.
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment