Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Thursday, July 20, 2017

Kesi ya Manji yaahirishwa

Yusuf Manji.

KESI inayomkabili aliyekuwa Mwenyekiti wa Klabu ya Yanga, Yusuf Manji imeahirishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jiji Dar hadi Agosti 4 mwaka huu kutokana na upelelezi kutokamilika.

Kesi hiyo inayoendeshwa na Hakimu, Huruma Shaidi ilikuwa isikilizwe leo lakini Manji hakufika mahakamani hapo kwa kile kilichoelezwa na mawakili wake kuwa ni mgonjwa na yupo Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete Muhimbili akitibiwa maradhi ya moyo.

Julai 5 mwaka huu, Manji akiwa amelazwa Muhimbili alisomewa mashtaka saba na watuhumiwa wenzake, yakiwemo ya uhujumu uchumi, kukutwa na mihuri miwili ya JWTZ, ukiwemo wa Mkuu wa Kikosi cha 21 JWTZ, wa Mkuu wa Kikosi Makutupora Dodoma (JWTZ) na wa Commanding Officer Korogwe, plate number mbili za magari ya serikali jambo ambalo nalo ni kinyume cha sheria.

Watuhumiwa wengine katika sakata hilo ni Deogratius Kasinda na Thobias Pwere na mtu mmoja ambaye jina lake halikufahamika mara moja na wote wamerudishwa rumande.
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment