Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Thursday, July 27, 2017

Coutinho aomba kwenda Barcelona

Bado dirisha la usajili linaendelea kushika kasika kasi na taarifa za chini chini zinadai kiungo wa Liverpool Phellipe Coutinho amemuomba kocha wake Jurgen Klopp amruhusu kwenda Barcelona.

Inafahamika kwamba Barca wanaihitaji sahihi ya Coutinho na wameshatuma ofa kwa Liverpool na wameshafanya mazungumzo na Coutinho ambaye yuko tayari kujiunga nao wakati wowote.

Taarifa nyingine za usajili ni kwamba baada ya habari kuzagaa kwamba Mbappe anakwenda Real Madrid sasa Pep Gurdiola maeingia katika mapambano na anataka kutoa kitita kikubwa zaidi kwa Monaco ili kumnasa Mbappe.

Kocha wa Chelsea Antonio Conte amesema kwa sasa Harry Kane ndiye striker anayemkubali sana nje ya Chelsea lakini hawezi kumnunua kwani ana uhakika bei yake kwa sasa itakuwa iko juu sana.

Kiungo Jack Wilshaire hataki kuondoka nje ya jiji la London na anaona kama Arsenal wataamua kumuuza ni bora wamuuze humo humo London huku West Ham ikitajwa kama sehemu ambayo anaelekea Wilshaire.

Makamu wa raisi wa Monaco Vadim Vasylev amezikatisha tamaa klabu zinazowataka Fabinho na Lemar kwa kusema kwamba wachezaji hao ni muhimu na ana uhakika watabaki.
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment