Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Thursday, April 27, 2017

Emmanuel Macron na Le Pen waongoza katika duru ya kwanza



media
Emmanuel Macron na Marine Le Pen waongoza katika uchaguzi wa urais Ufaransa
Emmanuel Macron anaongoza katika duru ya kwanza ya uchaguzi wa urais nchini Ufaransa kwa 23.7% ya kura, akifuatiwa na Marine Le Pen kwa 21.7%, kulingana na makadirio ya awali ya mshirika wetu Ipsos.
Wakati huo huo rais wa Ufaransa François Hollande amepongeza Emmanuel Macron kwa simu.
Kwenye ukurasa wake wa Face book, mgombea wa chama cha France Insoumise Jean-Luc Mélenchon amesema hajasahihisha " matokeo yaliyotangzwa kupitia uchunguzi," akibaini kwamba "matokeo ya miji mikubwa bado hayajajulikana."
Wapiga kura Milioni 47 wanaamua ni nani atakayemrithi rais Francois Hollande ambaye mwaka uliopita, alitangaza kutotetea nafasi yake.
Usalama umeimarishwa kote nchini humo kuhakikisha kuwa zoezi hili linafanyika na kumalizika salama.
Hata hivyo, wachambuzi nchini humo wanasema kuwa Marine Le Pen na Emmanuel Macron huenda wakamaliza katika nafasi ya kwanza na ya pili na kumenyana katika mzunguko wa pili.
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment