Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Wednesday, February 22, 2017

Mourinho asema Wayne Rooney anaweza kuondoka Manchester United


Rooney amekuwa Manchester United tangu 2004

Meneja wa Manchester United Jose Mourinho amesema bado inawezekana Wayne Rooney aihame klabu hiyo mwezi huu.

Mshambuliaji huyo wa England mwenye umri wa miaka 31 alifunga bao lake la 250 United mwezi uliopita na kuwa mchezaji aliyefunga mabao mengi katika historia ya klabu hiyo.

Hata hivyo, kumekuwa na uvumi kwamba huenda akahamia China.

Soko la kuhama kwa wachezaji Ligi Kuu ya China litafungwa wiki ijayo.

Mourinho aliulizwa iwapo nahodha huyo wa United atakuwa Old Trafford kufikia wakati huo.
"Itabidi mumwulize mwenyewe," Mourinho alisema.

"Bila shaka siwezi kuwahakikishia (kwamba atakuwa hapa). Siwezi kuwahakikishia kwamba nitakuwa hapa wiki ijayo, nitawezaje kuwahakikishia kwamba mchezaji atakuwa hapa msimu ujao?"
Mkataba wa Rooney United ni wa hadi 2019 na majuzi alikuwa amedokeza kwamba kuna uwezekano huenda asimalize muda wote huo United.

Amekuwa hapewi nafasi ya kuwa katika kikosi cha kuanza mechi msimu huu na amefunga mabao matano pekee.

Hata hivyo, Mourinho alisema Oktoba kwamba Rooney hakuwa anenda "popote" na alisisitiza Jumanne kwamba hataki mchezaji huyo aihame Manchester United.

"Siwezi kumsukuma - au kujaribu kumsukuma - nyota wa klabu hii ahame," aliongeza Mourinho.

"Hivyo, itabidi mumwulize iwapo anaona kama atakuwa katika klabu hii kipindi kilichosalia cha uchezaji wake au iwapo anadhani atahama.

"Si swali langu hilo kwa sababu ninafurahia kuwa naye. Sitaki aondoke
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment