Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Wednesday, February 22, 2017

Kiongozi wa zamani Hong Kong afungwa jela


Donald Tsang na mkewe Selina
 Kiongozi wa zamani wa Hong Kong Donald Tsang amehukumiwa kufungwa jela miezi 20 kwa kutumia vibaya mamlaka yake.

Tsang aliongoza Hong Kong kati ya 2005 na 2012 na ndiye afisa wa ngazi ya juu zaidi nchini humo kuwahi kushtakiwa kutokana na tuhuma za ulaji rushwa.

Alipatikana na hatia wiki iliyopita katika kesi iliyohusu nyumba ya kifahari nchini China.

Wakati wa kumhukumu, Jaji Andrew Chan alisema: "Daima, sijawahi katika kipindi changu kama jaji, kushuhudia mtu akishuka chini hivi kutoka kwenye upeo wa mamlaka."

Viongozi kadha wakuu wa zamani Hong Kong walikuwa wameandika barua kwa mahakama kumtetea Tsang.

Tsang aliondolewa makosa wiki iliyopita kuhusu shtaka la pili la kutumia vibaya mamlaka.
Tsang akiwasili kortini wakati wa kutolewa kwa hukumu
Jopo la waamuzi wa mahakama lilikosa kuafikiana kuhusu shtaka la tatu la kukubali manufaa kinyume cha sheria.

Baada ya kuhukumiwa, Tsang alitolewa kortini akiwa amefungwa pingu na kupelekwa hadi hospitalini ambapo amekuwa tangu Jumatatu baada ya kupatwa na maumivu ya kifua.
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment