Writen by
sadataley
3:37 PM
-
0
Comments
Msaidizi wa Mandela azua ubaguzi
Miaka 20 ya kuwa msaidizi wa Nelson Mandela na kuwa mfano mwema maridhiano ya rangi baada ya miaka mingi ya ubaguzi nchini Afrika Kusini imefutwa katika ujumbe wa mtandao wa Twitter.
Jamii ya Afrikaaner ilionekana kama ndio iliokuwa ikisukumu gurudumu la mfumo wa ubaguzi wa rangi.
Lakini iliwashangaza wengi baada ya ujumbe ulioandikwa katika mtandao wa twitter kutoka kwa msaidizi huyo wa kibinafsi wa marehemu Mandela kuonyesha kwamba alikuwa akipuuza madhara ya ubaguzi wa rangi na ukoloni miongoni wa raia wengi wa Afrika kusini.
Hivi ndivyo ujumbe huo ulivyosema.''Iwapo ningekuwa mwekezaji mweupe ningeondoka taifa hili.Ni wazi kutoka kwa rais Zuma kwamba watu weupe hawatakikani Afrika ya kusini'',.
Ujumbe huo ulizua hisia kali miongoni mwa raia huku baadhi ya wachanguzi weusi wa maswala ya kijamii wakisema kuwa sio kodi ya wazungu pekee inayojenga Afrika ya kusini.
Chanzo: BBC
No comments
Post a Comment