Writen by
sadataley
1:25 PM
-
0
Comments
BBC yazindua tuzo ya Komla Dumor
Shirika la habari la BBC linazindua tuzo kwa heshima ya aliyekuwa mtangazaji wake Komla Dumor, mwaka mmoja baada ya kifo chake akiwa na umri wa miaka 41.
Aliwakilisha Afrika kama bara lenye kujiamini na lenye wajasiri amali wengi.
Shirika la BBC limejitolea kuandeleza kazi ya Komla.
Tunajivunia sana kama BBC kutangaza tuzo ya uandishi wa habari kwa heshima ya aliyekuwa mwandishi mahiri wa BBC Komla Dumor
Tuzo hio itakuwa inatolewa kwa wandishi wenye kipaji wanaoishi barani Afrika na kufanya kazi barani humo. Sharti ni kwamba watakuwa wana kipaji cha hali ya juu kusimulia taarifa kuhusu bara la Afrika na pia wawe wanalenga kuwa mahiri katika siku za usoni.
Kupitia kwa tuzo hio,BBC itaweza kumleta mshindi katika shirika hilo kupata ujuzi wa kazi na kusimulia taarifa kuhusu Afrika kwa dunia nzima kwa kipindi cha miezi mitatu mjini London.
Mshindi pia atapata fursa ya kutangaza kwenye televishini , redio na kuandika taarifa ambazo zitachapishwa kwenye mtandao kwa mashabiki milioni 265 wa BBC kote duniani.
Chanzo:BBC
No comments
Post a Comment