Latest News

GNM Cargo

GNM Cargo
GNM CARGO & LOGISTICS

menu

Wednesday, November 19, 2014

Wanajeshi kulipwa madai yao Ivory Coast

   
Waziri wa mambo ya ndani wa Ivory Coast Hamad Bakayoko
Waziri wa mambo ya ndani wa Ivory Coast, Hamad Bakayoko ameahidi kuwa Serikali itashughulikia madai ya maelfu ya Wanajeshi walioandamana.
ametoa ahadi hiyo kwa njia ya Televisheni usiku wa jumanne baada ya Wanajeshi kufunga Barabara katika miji muhimu miwili.
Bayoko amesema Wanajeshi hawatawekewa vikwazo vyovyote kutokana na kuandamana kwao.
Madai ni ya Wanajeshi takriban 9,000 waliokuwa wapiganaji waasi ambao baadae walijiunga na Jeshi.
Wapiganaji hao walikua sehemu ya kikosi kinachomtii Rais Alassane Ouattara aliyechukua madaraka mwaka 2011, na kumaliza vita vya wenyewe kwa wenyewe.
Mapema siku ya jumanne,Waziri wa ulinzi Paul Koffi aliwataka Wanajeshi kurejea kambini baada ya kufunga barabara za mji wa Abidjan na Bouake.
Taarifa za jumatano zinasema Wanajeshi tayari wameondoka mjini Bouake.
Haya ni maandamano makubwa kuhusisha jeshi tangu Rais Alassane Ouattara kuchukua madaraka
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment