Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Wednesday, November 5, 2014

Rais wa Ukraine aahidi mabadiliko

   
Rais wa Ukraine Petro Poroshenko
Rais Petro Poroshenko, Ukraine ameitaka idara ya usalama na bunge la nchi hii kuiondoa sheria inayoruhusu kujitenga kwa maeneo mawili yaliyopo Mashariki mwa nchi hiyo.
Akizungumza muda mfupi baada ya mkutano wa baraza la usalama la nchi hiyo Poroshenko amesema amewaagiza baadhi ya makamanda kupeleka vikosi vyao katika eneo hilo ili kujikinga na mashambulio katika eneo hilo.
Amesema kuwa upo uwezekano wa waasi wanaosaidiwa na Urusi kuweza kufanya mashambulizi katika mji wa pili kwa ukubwa wa Kharkiv na Bandari ya Mariupol.
Hata hivyo hatua hii ya Rais Poroshenko inakuja huku siku ya jumapili waasi wa mashariki wa Ukraine walifanya uchaguzi katika majimbo ya Donetsk naJamhuri ya Luhansk.
Ukraine nan chi za Mahgharibi wametangaza kuwa uchaguzi huo si halali lakini Urusi inaonekana kuegemea kwa waasi hao Zaidi.
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment