Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Saturday, November 8, 2014

IGAD yaipa S-Sudan wiki mbili.

    Viongozi wa IGAD
Pande mbili zinazopigana Sudan Kusini zimepewa siku 15 zaidi kumaliza vita vya karibu mwaka, na kuhitimisha makubaliano ya kugawana madaraka.
Iwapo hazikufanya hivyo, basi pande hizo mbili zitawekewa vikwazo na mataifa mengine ya Afrika Mashariki.
Msemaji wa Jumuia ya nchi za Pembe ya Afrika, (IGAD) alieleza kuwa baada ya mazungumzo ya siku mbili mjini Addis Ababa, pande zinazopigana Sudan Kusini zimekubali kusitisha vita moja-kwa-moja.
Pande hizo zilionywa yatayofwata iwapo zitavunja makubaliano, kama alivotamka msemaji wa IGAD.
"Makubaliano ya kusitisha mapigano yakivunjwa na upande wowote ule, hatua zinazofuata zitachukuliwa na Jumuia ya IGAD:
Mali za pande hizo zitazuwiliwa.
Wanasiasa watapigwa marufuku kusafiri katika eneo la IGAD
Silaha na risasi zitazuwiliwa kupelekwa Sudan Kusini, pamoja na zana zote zinazoweza kutumiwa kwenye vita"
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment