Latest News

GNM Cargo

GNM Cargo
GNM CARGO & LOGISTICS

menu

Sunday, October 19, 2014

Joto uchaguzi Serikali za mitaa lapanda


Waziri Mkuu,Mizengo Pinda 
Na Beatrice Moses, Mwananchi
Dar es Salaam. Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi) imetangaza ongezeko la idadi ya kata, vijiji, mitaa na vitongoji nchini vitakavyotumika kwa ajili ya uchaguzi serikali za mitaa, huku hatua hiyo ikiibua hoja miongoni mwa wanasiasa na wasomi.

Tayari vyama vya siasa vimeanza kufanya maandalizi ya uchaguzi huo wa serikali za mitaa unaotarajiwa kufanyika Desemba 14, mwaka huu. Wanasiasa na wasomi wametoa maoni yao kuhusu hatua hiyo, wengi wakilalamikia jinsi isivyokidhi mahitaji ya wananchi na wengine wakielezea kuwa imetangazwa wakati huu kuwanufaisha wachache ili wapate madaraka.

Akizungumza na gazeti hili, Mkurugenzi wa Serikali za Mitaa Ofisi ya Waziri Mkuu, Kalist Luanda alisema Serikali imeongeza idadi hiyo ili kuanzisha maeneo mapya ya kiutawala ambayo yatawawezesha wananchi kupata huduma za kijamii na kiutawala kwa karibu.

Alisema ongezeko hilo limefanywa kwa kuzingatia idadi ya watu kuongezeka kwa kasi na kupanuka kwa maeneo baada ya watu kujisajili, hivyo kata zimeongezwa na kuwa 465, vijiji 628, mitaa 746 na vitongoji 4,257. Kata kwa nchi nzima zimeongezwa kutoka 3,802 mwaka 2009 hadi 3,337, vijiji vimeongezeka kutoka 11,795 hadi 12,423 na mitaa imetoka 2,995 hadi 3,741 kwa upande wa vitongoji imeongezeka kutoka 60,359 hadi 64,616.
Nape

Hata hivyo, Katibu wa Itikadi na Uenezi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Nape Nnauye akizungumzia uamuzi huo aliikosoa hatua hiyo akieleza kwamba idadi ya vijiji vilivyoongezwa ni ndogo ikilinganishwa na mahitaji yaliyopo.

“Kuna malalamiko mengi kuhusu vijiji hata hivi karibuni kwenye ziara huko Iringa tulifikishiwa malalamiko hayo bado hatujapata uhakika wa vigezo vilivyotumika kuongeza idadi ya vijiji hivyo na kwamba kwa kata mimi sina shida,” alisema.

Nape alisema hata kwenye mkutano wa Halmashauri Kuu ya CCM, wajumbe wengi walitoa malalamiko yao kuhusu maombi ya vijiji, ingawa kuna maelezo ya awali yaliyotolewa na Serikali kuhusu kukwamishwa na gharama za kuwalipa viongozi wa ngazi hizo.

“Hii bado siyo sababu ya kujitosheleza nafikiri Serikali ichukue hatua ya kuongeza vijiji zaidi, bado ina nafasi ya kufanya hivyo kabla ya uchaguzi wa serikali za mitaa, gharama inazosema nafikiri madiwani kupitia halmashauri zao walivipitisha baada ya kutambua kuwa watazimudu,” alisema Nape.
Akizungumzia jinsi CCM ilivyojidhatiti kushinda katika uchaguzi huo alisema kwamba, watashinda karibu mitaa yote kwa asilimia 96, hasa kwa kuwa upinzani wamejiunga na kuwa Ukawa, itakuwa ngumu kwao kujipanga na kushinda.

Dk Slaa

Katibu Mkuu wa Chadema, Dk Wilbrod Slaa alisema kuwa anatarajia kufanya utafiti ili kujua ongozeko hilo kama lilifanywa kwa kuzingatia utaratibu unaostahili au umefanywa kwa manufaa ya mtu binafsi.
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment