Writen by
sadataley
2:12 PM
-
0
Comments
Kiongozi wa zamani wa Cuba Fidel Castro
Cuba ina historia ya kupeleka madaktari wake kote duniani inapotokea dharura.
Kiongozi wa zamani wa Cuba Fidel Castro, anasema taifa hilo la visiwa vya Carribean litashirikiana “kwa nia njema” na Marekani katika kupambana dhidi ya ugonjwa wa Ebola huko Afrika Magharibi.
Mtangazaji wa televisheni ya Cuba alisoma ujumbe wa maandishi wa bwana Castro hewani.
Siku ya Ijumaa waziri wa mambo ya nje wa Marekani John Kerry alisifu juhudi za Cuba kufuatia mlipuko wa Ebola, akisema kuwa “Cuba,nchi ya watu milioni 11na imepeleka wataalam wa afya 165, na ina mpango wa kupeleka wengine takriban 300” kuisaidia nchi za Afrika Magharibi zilizoathiriwa zaidi.
Cuba ina historia ya kupeleka madaktari wake kote duniani inapotokea dharura.
No comments
Post a Comment