Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Saturday, August 9, 2014

Hatimaye Rodriguez apokea tuzo

Hatimaye James Rodriguez ametuzwa tuzo la mfungaji bora.
Hatimaye mshambulzi wa Colombia James Rodriguez aliyeduwaza ulimwengu kwa kufunga mabao mengi zaidi katika kombe la dunia lililokamilika huko Brazil mwezi uliopita amepokea tuzo lake la mfungaji mabao mengi '' Golden Boot''.
Rodriguez ambaye aliyetikisa wavu mara 6 huko Brazil sasa anakibarua cha kutafuta namba huko Real Madrid dhidi ya wakinzani wenye haiba yake kama mchezaji bora msimu huu Christiano Ronaldo.
Rodriguez alinunuliwa na mabingwa hao wa kombe la mabingwa barani ulaya kutoka Monaco kwa pauni milioni 71.
Mshambulizi huyo mwenye umri wa miaka 23 alisema kuwa anamatumaini makubwa ya kutamba Santiago Bernabéu.
James Rodriguez akilia baada ya kushindwa na Brazil.
Bao lake dhidi ya Uruguay katika robo fainali ya kombe la dunia limepigiwa upatu kutwaa tuzo la bao la mashindano japo Rodriguez mwenyewe anaikumbuka bao lake la kipekee dhidi ya Japan kuwa bora.
Colombia ilitegemea mabao yake sita katika mechi 5 kufuzu kwa hatua ya robo fainali kabla ya kuambulia kichapo cha 2-1 dhidi ya wenyeji Brazil.
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment