Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Saturday, August 9, 2014

AU itaunda kitengo cha magonjwa


Udhibiti wa Ebola, Nigeria
Mwenyekiti wa Hamashauri ya Umoja wa Afrika, Nkosazana Dlamini-Zuma, ametoa wito kwa nchi za Afrika na duniani kote kushirikiana kuzuwia ugonjwa wa Ebola uliosambaa Afrika Magharibi, usitapakae kwengineko.
Shirika la Afya Duniani, WHO, linakisia kuwa watu kama 960 wamekufa kutokana na Ebola huko Guinea, Sierra Leone, Liberia na Nigeria.
Nkosazana Dlamini-Zuma alisema nchi za Afrika zinataraji kuunda kitengo cha pamoja kupambana na ugonjwa huo:
"Nchi za Afrika zimefikia uamauzi kuwa tunataka kuanzisha kitengo cha kudhibiti magonjwa.
Na tutafanya kazi pamoja na washirika wetu.
Marekani imekwishasema kuwa iko tayari kushirikiana nasi, lakini siyo pekee.
Lazima tushirikiane sana na WHO katika swala hili na washirika wengine walio tayari kuwa nasi"
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment