Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Wednesday, July 23, 2014

Rodriguez atua Bernabeu kwa miaka 6

Real Madrid imemnunua James Rodriguez
Mshambulizi wa Colombia na Monaco James Rodriguez amezunduliwa kama mchezaji wa Real Madrid baada ya kutia sahihi kandarasi ya miaka 6 na mabingwa hao wa bara Ulaya.
Mchezaji huyo wa aliyetwaa taji la mfungaji mabao mengi katika kombe la dunia huko Brazil ameandikisha kandarasi ya miaka 6 na klabu hiyo.
Duru zinaiarifu BBCMichezo kuwa huenda James akapokea kitita cha dola milioni mia moja.
Kutua kwake huko Bernabeu kumemuweka Rodriguez katika mizani sawa na Gareth Bale, Cristiano Ronaldo na Luis Suarez.
Real Madrid imemnunua James Rodriguez
Iwapo Rodriguez atalipwa takriban pauni millioni 80 basi huenda atakuwa mchezaji wa nne ghali zaidi nyuma ya Bale, Ronaldo na Suarez.
Rodriguez aligonga vichwa vya habari baada ya kutinga mabao 6 licha ya timu yake ya Colombia kubanduliwa nje ya kombe la dunia katika hatua ya robo fainali.
Rodriguez alifunga mabao dhidi ya Ugiriki , Ivory Coast na Japan lakini atakumbukwa zaidi kwa bao lililopigiwa upatu kuwa bora zaidi katika mashindano hayo dhidi ya Uruguay.
Kabla ya kujiunga na Monaco Rodriguez alikuwa amedhihirisha udeddea wake huko Ureno alikotwaa mataji matatu ya ligi akiwa na klabu ya Porto.
Real Madrid imemnunua James Rodriguez
Naibu mwenyekiti wa wa klabu ya Monaco Vadim Vasilyev alisewaambia wanahabari kuwa klabu hiyo haikuwa na niya ya kumuuza mshambulizi huyo lakini hawakutaka kupitwa na kitita kikubwa kilichotolewa kwao na kumweka katika mizani sawa na washambulizi ghali zaidi katika hstoria ya kandanda.
Madrid ilitoa kitita cha pauni milioni 80 kumnunua Ronaldo alipotokea Manchester United mwaka wa 2009.
Na ulimwengu na kandanda ulipodhania kuwa historia hiyo haingevunjwa Madrid ilitoa pauni milioni 85.3m mwaka uliopita na kumnunua Bale kutoka kwa Tottenham ya Uingereza.
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment