Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Thursday, July 24, 2014

Michezo ya Jumuiya ya Madola kuanza-Glascow

Nembo ya mashindano ya Jumuiya ya madola
Nembo ya mashindano ya Jumuiya ya madola
Mashindano ya Jumuiya ya Madola kuanza leo mjini Glascow Scotland na kufunguliwa rasmi na Malkia Elizabeth wa Uingereza ambaye pia ni mkuu wa nchi wanachama wa Jumuiya ya madola.
Zaidi ya wanariadha elfu tatu wanatarajiwa kushiriki katika mashindano hayo yatakayodumu kwa muda wa majuma matatu yajayo.
Australia ndio nchi ambayo imetuma kikosi kubwa zaidi katika mashindano haya ya mwaka huu.
Takwimu rasmi zinasema kuwa Australia inaakilishwa na zaidi ya wanariadha 400.
Wanariadha wakijipasha misuli kabla ya kuanza kwa mashindano
Mataifa yote nchi wanachama wa muungano huo kutoka kanda ya Afrika Mashariki na Kati yameakilishwa kwenye mashindano ya mwaka huu.
Ushindani mkali unatarajiwa katika fani mbali mbali za michezo na macho yote ya dunia itakuwa katika shindano la riadha ambalo litatumiwa na mataifa mengi kuchagua vikosi vyao vitakavyoshiriki katika mashindano ya mabara na hatimaye kombe la dunia.
Mashindano haya yataanza rasmi hiyo kesho huku wanariadha kadhaa wa Afrika Mashariki wakijibwaga ugani kuchuana na wapinzani wao katika raundi ya kwanza ya mashindano ya Judo, Masumbwi na Table tennis.
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment