Latest News

GNM Cargo

GNM Cargo
GNM CARGO & LOGISTICS

menu

Wednesday, June 11, 2014

Mangula akiri kuwapo kwa mpasuko TCD


Makamu mwenyekiti wa Kituo cha Demokrasia Tanzania (TCD), Philip Mangula.PICHA|MAKTABA 
Na Fidelis Butahe na Edwin Mjwahuzi, MwananchiDodoma. Makamu mwenyekiti wa Kituo cha Demokrasia Tanzania (TCD), Philip Mangula amesema kituo hicho kimekumbwa na mpasuko baada ya vyama vya Chadema na CUF kususia kikao kilichoitishwa Jumapili iliyopita.
Kitendo cha vyama hivyo kutoonekana kumetafsiriwa kama mwendelezo wa kile kilichotokea katika Bunge Maalumu la Katiba Aprili 16, baada ya wapinzani kususia vikao kutokana na kutokuridhishwa na mwenendo wa chombo hicho.
Akizungumza na waandishi wa habari jana katika ofisi za makao makuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) mjini hapa, Mangula ambaye pia ni makamu mwenyekiti wa CCM, alisema kikao hicho kililenga kujadili mwenendo wa vyama na athari zake kisiasa.
Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe alisema viongozi wa vyama vya siasa huitwa kwa mialiko. “Sikuona ulazima wa Mangula kukimbilia katika vyombo vya habari na kuzungumza jambo hili,” alisema. Mbowe alisema Chadema na CUF si wanachama pekee wa TCD.
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment